Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Wednesday, November 8, 2023

HURUMA INAYOUMA-Utangulizi


'Docta, huyu sio mtoto wangu, ….’akasema mdada.

‘Sio mtoto wako…! ' Akasema docta kwa mshangao, na mdada akawa kimia

'Kama sio mtoto wako, wazazi wake wapo wapi…au wewe ni nani kwake?’ docta akauliza, akiangalia saa yake, akikumbuka anahitajika kwenda wodini kuna mgonjwa alihitajia huduma yake.

‘Docta mimi ki-ki ukweli, s-sijui, hutaamini lakini sijui….’kauli iliyomfanya docta aweke peni mezani, akaangalia simu ya mezani, akitarajia kuitwa muda wowote.Lakini  kwa kauli hiyo ya mdada ilimfanya ahisi kuna jambo linakuja.

Docta akaangalia saa yake tena,….halafu akamwangalia yule mdada, hakuweza kuona sura ya huyi mdada vyema kwani kwa muda ule huyo mdada alikuwa kainamisha kichwa chini. Docta akamuangalia mtoto aliyebebwa na huyo mdada, halafu akamuangalai  tena yule mdada. Docta alitafuta jambo kwa wawili hao, huku akichelea muda…!

‘Unajua sikuelewi, kama wewe sio mzazi, wewe ni nani kwa huyo mtoto…?’ akauliza docta

‘Docta , naomba tu unielewe, mimi sijui wazazi wake wapo wapi, mtoto anaumwa, ni huruma ..ni…huruma yangu tu….’akasema sasa huyo mdada kwa sauti ya huzuni.

‘Sawa…lakini kwanza unielewe… ili mtoto atibiwe, eeh, si tunahitaji maelezo, eeh….kwanza kadi yake ya kliniki unayo..?’ akauliza docta

‘Si nimekuambia mimi siwajui wazazi wake, …mimi sina kadi yake… na hata sijui kama ana kadi….’akasema mdada

Docta akahema kama kuchoka hivi….akaangalia saa yake ya mkononi, halafu akataka kama kusimama, akaangalia simu ya mezani…ni kama alitaka kuitumia, au kusubiria kuitwa, akamuangalia mdada…

‘Mdada..!, sijui nikuite hivyo,...sijui kama unanielewa, na sijui kama tutaelewana, huyu ni mtoto mdogo, unasikia sana….umempataje mimi sijui eeh…si wewe umekuja naye, au..?’akasema docta lakini mdada alimkatisha kwa kauli iliyomshfanya docta agwaye kudogo

‘Docta,….naomba msaada wako..!’akasema mdada.

 Msaada….!

Docta kusikia hiyo kauli akilini akasema,…yah…kama nilivyowaza, yale yale….!

Lakini docta hakutaka kulichukulia hilo analoliwaza akilini kwa haraka, kwanza akavuta subira, akawa anamuangalia yule mdada,….mdada alikuwa kimia, bado akiwa kainamisha kichwa chini akimuangalia yule mtoto.

‘Msaada…!, unaomba msaada gani…?’ akauliza docta

Mdada aliendelea kukaa kimia,… halafu baadae yule mdada akainua kichwa na kumtizama docta, mara moja paah…halafu akarudisha macho chini.

Docta aliyaona yale macho, yale macho yalikuwa kama  yanalengwa lengwa na machozi. Hata hivyo, docta hakuweza kumuona vyema,…Hata hivyo,Docta machozi ya wagonjwa ameyazoea!

Docta kwa uzoefu wake, akahisi kuna jambo, na hayo machozi sio kama yale aliyoyazoea, hata hivyo,aliona avute subira, hakuwazia tena huyo mgonjwa mwingine wa wodini,…

Kuna jambo kwa huyo mdada na mtoto….Aliwaza hivyo!

Yule mdada sasa taratibu akainua uso, na sasa akamtizama docta, moja kwa moja, macho ya mdada yakakutana na macho ya docta, hapo sasa ndio docta akaweza kumuangalia vyema huyo mdada, na machoni kulikuwa kukavu,

Mhh...…. Docta aliguna hivyo kimoyo moyoni

‘Docta, ninaomba umtibie tu huyu mtoto tujue ana shida gani….hilo tu docta….’akasema huyo mdada, kabla docta hajahitimisha uchunguzi wake wa kuwalinganisha wawili hao kama kuna uhusiano wowote mdada aliongea hivyo .

Docta, kwa haraka akachukua peni na kuandika kitu kwenye kadi, halafu…

Na mara simu ya mezani ikaanza kulia…


NB. Ni tukio nililokutana nalo hospitalini, na diary yangu ikaona sio vyema lipite bure.....Ni kisa cha mdada na mtoto, Je huruma yake iliishia wapi? Je kuna nini nyuma ya pazia.....

KARIBUNI SANA KWENYE SEHEMU YA INAYOFUATA



i mimi: emu-three

Friday, September 22, 2023

TUSAIDIE TUPATE BARAKA


Nikiwa nimekaa ndani ya gari la daladala, macho yangu yalivutiwa na abiria wanaogombea kuingia ndani ya dala dala hilo. 

Abiria wanaotaka kuingia walikuwa wengi zaidi ya uwezo wa gari hilo....kwahiyo ilikuwa mshikemshike, na kati ya hao abiria, nilimuona mtoto , nahisi anaweza kuwa kati ya miaka mitano au sita, akiwa na sare zake za chekechea nahisi

Kwa vile abiria walikuwa wengi, na kila mmoja anataka kuwahi kuingia, hakuna aliyemjali huyo mtoto, walimsukumia nje...lakini yule mtoto akawa naye anajitahidi kushindana ili naye awahi kuingia, kwa bahati mbaya akadondoka chini

Hakuna aliyemjali....walioweza kuingia wakaingia, na wengine wakabakia nje, sasa wale waliobaki nje ndio wakamuona huyo mtoto, ...

'Vipi umeumia..?' mmoja wa abiria akamuuliza
 Yule mtoto akawa analia...huku akijifuta futa, na kuokota mkoba wake wa madafutari, na bado akijaribu kuona kama ataweza kuingia

''Endesha gari....' konda wa hilo dala dala akasema, bila kujali kuwa kuna mtoto alianguka, na hakutaka hata kumsaidia angalau aingie

Baadhi ya abiria walioingia ndani wakawa wanamsema konda, asimamishe garii amchukue huyo mtoto

'Wanafunzi wameingia wengi sana, na hata akiingia atakaa wapi...'akasema konda na dala dala likwa limeingia barabara kuu, mtoto akabakia kituoni na abiria wengine.

Hatukifika mbali gari likakamatwa na trafiki kwa makosa ya kupitia njia za mkato...ikawa ndio mwisho wa safari hiyo, kwasababu trafiki alisema hilo gari sio mara ya kwanza, kahiyo linahitajika kituo cha polisi

WAZO LA LEO: Wakati mwingine tunazikataa baraka zetu sisi wenyewe...tuwasaidie wenye shida, kwani kutokana na wao, ndipo baraka zilipo.
Ni mimi: emu-three

Friday, September 8, 2023

NI KIPI KIPYA NIJIFUNZE...


KIPI KIPYA!

Niandike nini ambacho hakijawahi kuandikwa, niseme nini ambacho hakijawahi kusemwa, nione kitu gani kipya ambacho hakijawahi kuonwa, nisikie nini kipya ambacho hakijawahi kusikiwa....nahisi kila kitu kina msingi, ...na sie ni waendelezaji tu, labda, taaluma na mitandao ambayo inakuwa kila siku , lakini hata yenyewe ina asili yake!

Ni mimi: emu-three


Tuesday, June 27, 2023

JINAMIZI.....Utangulizi..

Ilipoanzia....

Nilishtuka toka mawazoni, kilichonishtuka ni sauti....

Sauti ya mtu analia...nikageuka kushoto kwangu, kama vile vile...sauti kama ile ile, kiukweli niliogopa kugeuka, hata hivyo, nikafanya kama vile..

'Unalia nini..?'

Abiria yule akawa kama kashtuka, kwa haraka akanitupia jicho, macho yangu yakakutana na yake, ...akawa kama kashtuka fulani hivi...akashika mdomoni,....kama haamini, kama ....nahis hivyo, sasa  akawa kama anawaza jambo fulani, halafu akasema

'Siamini...'

Kimia kikatanda,  na niliyemuuliza akawa anajifutafuta usoni na leso, na kujifanya kama vile kuna kitu kilimuingia machoni, halafu akarudia tena kusema...

'Siamini...!' halafu akashika kichwa na kuinama kama anawaza jambo...halafu taratibu akainua uso kuniangalia, sasa akiwa katoa jicho la woga......

Mdada mrembo...sasa tulipokutanisha macho yetu,..hii ni mara ya pili, mimi sasa... nilihisi moyo kunienda mbio, mwili ukaisha nguvu.....sijui kwanini

Nilikuwa na yangu kichwani, kichwa kilikuwa kinauma kwa mawazo..
,..na kwa hili, kichwa kikazidi kuuma....kukapita ukimia fulani,...na nili-nilipoona hivyo, kwa maana sasa mdada aliinamisha kichwa chini na mimi sasa nikaona nijinyamazie tu,  nilitafakari hili jambo.

Yaliyokuwa kichwani sasa yalikuwa ni lukuki....

'Kama  hii ni kweli ni heri nife tu....'kauli ndogo ikasikika.

Hapo sasa niligeuza kichwa upande ule wa kushoto kwangu  huyo mdada....sasa akiwa kaangalia mbele tu, ni kama kazama kwenye dimbwi la mawazo.

Kimia kikapita tena...na nikaona labda yamepita, lakini haikupita muda, nikahis huyu mdada analia...

Sikuweza kuvumilia

'Samahani, ...naona hata nikivumilia sitakuwa na amani..dada tafadhali ninambomba sana...uniambie wewe ni nani...na na... niambie yaliyokusibu, huenda tukasaidiana..

'Mhh....'akaguna hivyo

'Naona unalia, na nimesikia neno aheri nife tu.....kwanini....'

Hapo akageuza kichwa kuangalia dirishani,...sasa akionyesha wasiwasi...ni kama anataka kutokea dirishani hivi... 

'Ha-ha...hamna kitu...'akasema hivyo sasa kidhahiri anaogopa, je anaogopa nini...ananiogopa mimi,...!

'Hamna kitu , wakati hali inaashiria kuna jambo....huwezi jua labda kukutana mimi na wewe kuna sababu, huenda tukasaidiana ukaja kunishukuru....tuka...'

'Wala usihangaishe kichwa chako, kuniwaza mimi....nahis hii ndio hatima yangu,...labda, ...sistahili kuishi,...niache tu....isije ikawa ni kweli.....labda ni wewe....'hapo akaendelea kulia, sasa akiwa kajiinamisha kichwa.

Niligeuka huku na kule kuwaangalia abiria wengine, labda kuna mtu anafuatilia haya mazungmzo, lakini wengi walitingwa na mambo yao, na asubuhi kama hii kila mtu ana jambo lake.

'Wale wa mnazi mmoja...'konda akanadi, nami nikajua baada ya vituo kadha nitakuwa nimefika mwisho wa safari yangu, lakini sikuwa na amani moyoni..

'Nikuulize tu....sasa unakwenda wapi?'

'Kujitosa baharini....'akasema na hapo nikashituka, 

'Wewe.....binti mrembo kama wewe unataka kujitosha baharini, kwa jipi kubwa, unajua nikuambie kitu, ujana ni pambio, na katika ujana mengi yanapita, na yatapita utayasahau,...muhimu kama kuna changamoto fulani, ichukulie kama mtihani tu...ukifeli, bado maisha yapo...

'Hahahaha.....ulisema hivyo hivyo....hahaha....nilijua ni ndoto ya jinamizi lakini ...nahisi ni kweli...nahisi...mungu wangu nifanye nini mimi, ....'akasema 

Nifanyeje....

'Sikiliza mimi nateremka posta, tukifika hapo posta, tuteremke pamoja, tukae mahali tuongee, ....

'Tuongee nini....'akasema kwa hasira

'Kuhusu matatizo yako..'

'Matatizo yangu....wakati wewe ndio chanzo cha yote...'akasema kwa hasira

'Mimi ndio chanzo cha yote kwa vipi...'

'Hahaha...unajifanya hunikumbuki sio....'akasema

'Sasa unanichanganya naona haupo sawa...'nikasema ...sasa nikitaka kuachana na huyo mdada, nilihisi huenda ana amatatizo kichwani

'Unakumbuka jana ulikuwa wapi usiku...?' akaniuliza

'Jana.!!.......'nikasema sasa nikishtuka,...ilinifanay nigeuza kichwa taratibu kuangalia huku na kule kama watu wanasikia, au kufuatilia.

'Kumbuka.....ulipoamuka subuhi, ulikuwaje..?' akaniuliza

Hapo nikagwaya...kwa maana awali nilitingwa na yangu kichwani, kwa maana nilijua ni ndoto tu, sasa mbona ...

'Mimi naenda kujiua,...lakini hutaishi salama.....'akasema

'Mimi sielewi kitu...'nikasema na .....

'Posta...posta......'konda akasema na nikajua nimeshafika mwisho wa safari yangu, ....lakini je niliache hili jambo hivi hivi, au....

'Teremka umeshafika, ...kumbuka tutakutana kuzimu,....sio ndoto ile,.....'akasema mdada

**************


Ni mimi: emu-threeH

Wednesday, May 10, 2023

NIMLILIE NANI....

                                                  NIMLILIE NANI....


Nilishika shavu, nikiwa nimeinamisha kichwa chini, kichwa kikiwa karibu ya magoti...nilikuwa hivyo kwa muda, baadae nikainua kichwa kujaribu kuangalia mbele, macho hayakuweza kuona,...macho bado yalikuwa yakilengwa lengwa na machozi, Lakini machozi hayakuweza kutoka tena...moyoni nilishaapa sitalia tena.....

'Sitalia......inatosha....basi...'

Nilijaribu kugeuza kichwa kushoto na kulia...japo ni kwa shida maana shingo ilikuwa kama imekakamaa...kiukweli sikuweza kuona kitu, zaidi ya ukungu, sio ukungu wa hali ya hewa, nahisi ni ukungu wa macho yangu...

Nilihisi mwili kuishiwa nguvu....moyo kwenda kasi, na kichwa kikazidi kuuma, sasa kikiuma kwa kasi zaidi,....ghafla...giza likanijia, na hatimaye ....

'Vipi kaamuka...?
Ilikuwa sauti ya kwanza kuisikia baada ya kupoteza fahamu, nahisi nilipoteza fahamu, au,...sina uhakika!

'Nahisi hivyo, japo hajafumbua macho...'sauti nyingine ikasema

'Usimsumbue kwanza, ngoja nikamuite docta..,usiondoke hapo,....'sauti nyingine ikasema

Hapo nikajitahidi kufumbua macho....

Ni mimi: emu-three